Mahakama ni mahali rasmi na pa bila mchezo. Watu wanatarajia kuwa na tabia inayoonyesha heshima kwa Mahakama na mfumo wa haki.
Wakati wowote Hakimu anapoingia au kuondoka chumba cha mahakama, unapaswa kusimama na kuinamisha kichwa chako. Wakati wowote unapoingia au kuondoka chumba cha mahakama, unapaswa kuinamia Nembo ya Queensland. Unapaswa kuita Hakimu kwa jina la “Mheshimiwa” na kusimama wakati wowote Hakimu anapozungumza nawe.
Inatarajia kwamba watu wale ambao wako kwenye chumba cha mahakama watakuwa kimya na wenye heshima. Usiongee isipokuwa umeitwa kusema na Hakimu. Usile, kuvuta sigara, au kutafuna gamu.
Unapokuwa kwenye chumba cha mahakama, hakikisha simu yako imezimwa au imewashwa kuwa kimya. Lazima usipige picha au kurekodi kesi.
Tovuti ina habari zaidi kuhusu kwenda mahakamani na huduma za mahakama. Pia ina idadi ya viungo vya nyenzo nyingine zinazosaidia.